Sunday, December 27, 2015

WAZIRI MKUU KUNUSURIKA AJALI YA NDEGE LEO 27/12/2015


Waziri mkuu wa Benin, Lionel Zinsou, anasemekana kuwa salama baada ya ndege ya helikopta

Thursday, December 24, 2015

MILIONI 18 TAHABANI KWA EL- NINO AFRIKA MASHARIKI



Wataalam wanasema kwamba watu wasiopungua milioni 18 katika upembe wa Afrika wameathirika na ukame unaotokana na mfumo wa hali ya hewa ya El-Nino.
Mamlaka ya Maendeleola ya Kimataifa IGAD , na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu imeonya kuwepo kwa upungufu mkubwa wa fedha ya kukabiliana na athari za El-Nino.
Watabiri wa hali ya hewa walitabiri athari kubwa kutokana na mvua ya El-Nino kwa miongo kadhaa sasa.




Monday, December 14, 2015

FURAHA YA MAASKOFU KUTOKA KWA MAKAMU WA RAIS KATIKA TAMASHA LA KRISMASI


tanzania-bishop-malasusa
Na Mwandishi Wetu
MAASKOFU wa madhehebu  mbalimbali wa Makanisa hapa Tanzania wamempongeza Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan kukubali kuwa mgeni rasmi katika Tamasha la Krismasi linalotarajia kufanyika Desemba 25 kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.
Tamasha hilo linalokwenda sambamba na Shukrani kwa Mungu baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 25 kwa amani na utulivu, uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Askofu wa Kanisa la KKKT, Dk Alex Malasusa anasema ni jambo jema kumshukuru Mungu baada ya uchaguzi Mkuu uliofanyika kwa amani na utulivu kiasi cha kumpata rais mchapakazi.

Sunday, December 13, 2015

TANESCO TUMBO JOTO LEO

DAR ES SALAAM.Sospeter Muhongo,waziri wa nishati na madini

Serikali imeliagiza Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuacha mara moja tabia ya kukata umeme bila sababu ya msingi.
Agizo hilo limetolewa jana jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo na Naibu wake, Dkt Medard Kalemani walipofanya ziara ya kushtukiza kwenye Ofisi za Makao Makuu ya Wizara hiyo.
Mara tu baada ya kuapishwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Naibu wake, Dkt Medard Kalemani walifanya ziara hiyo ya kushtukiza kwenye Ofisi za Makao Makuu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na kuzungumza na Menejimenti ya Shirika hilo.
Profesa Muhongo alisema wananchi wamechoshwa na tabia ya shirika hilo ya kukatakata umeme bila kuwepo na sababu ya msingi ya kufanya hivyo.
Haiwezekani kila mwaka matatizo ni yaleyale na nyie bado mpo ofisini, hili halikubaliki na

Saturday, November 21, 2015

MIILI YA WATU 18 KUPATIKANA HOTELINI


Mali
Polisi wa Mali wameingia katika hoteli hiyo
Maafisa wa serikali ya Mali wamesema sasa hakuna mateka wowote waliosalia katika hoteli ya Radisson Blu mjini Bamako iliyokuwa imeshambulia asubuhi na watu wenye silaha huku miili ya watu 18 ikidaiwa kupatikana ndani ya hoteli hiyo.
Waziri wa usalama wa Mali Salif Traore ameambia kikao cha wanahabari kwamba watu wenye silaha walioshambulia hoteli ya Radisson kwa sasa hawazuilii mateka wowote.

Sunday, November 08, 2015

NI SABABU GANI ILIMLETA TB JOSHU TANZANIA?


Alipokelewa na Dkt. John Pombe Magufuli kabla ya kuapishwa kuwa Rais wa awamu ya

KWELI WE JEMBE LETU

Rais Dkt. John Pombe Magufuli akifanyakazi ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam siku ikiwa ni siku yake ya kwanza ofisini kwake tangu alipoapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wa awamu ya tano. 

Achagua Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Monday, October 26, 2015

HONGERA WATANZANIA KWA USHINDI MKUBWA

-Ni Uchaguzi Wetu Wa Amani, Ni Ushindi Wetu..!
Ndugu zangu,
Macho ya dunia yanaiangazia nchi yetu kwa sasa.
Ndio, dunia inaiangalia Tanzania kama kielelezo cha taifa la Kiafrika lililodumu kwa zaidi ya nusu karne bila uwepo wa machafuko na watu kuuana kama ilivyo kwa maeneo mengine ya Afrika.
Tuna kila sababu za kuionyesha dunia, kuwa tunaweza kufanya chaguzi za kidemokrasia bila wenye

Friday, October 23, 2015

ZUMA KUKUTANA NA WANAFUNZI WANAOANDAMANA

 




  Baadhi ya wanafunzi wamepanga kuandamana hadi afisi kuu za serikali Pretoria
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amepangiwa kukutana na viongozi wa wanafunzi wa vyuo leo kujadili maandamano ya wanafunzi yaliyosababishwa na kuongezwa kwa ada ya masomo.
Wanafunzi wamekuwa wakiandamana wiki moja sasa, hasira nyingi zikielekezwa kwa chama tawala African National Congress (ANC).
Mnamo Alhamisi, maelfu ya wanafunzi walikusanyika nje ya makao makuu ya ANC mjini Johannesburg wakitaka elimu itolewe kwa wote bila malipo yoyote.
Vyuo vikuu vimejitetea na kusema vimelazimika kuongeza karo ili kudumisha viwango