Monday, October 26, 2015

HONGERA WATANZANIA KWA USHINDI MKUBWA

-Ni Uchaguzi Wetu Wa Amani, Ni Ushindi Wetu..!
Ndugu zangu,
Macho ya dunia yanaiangazia nchi yetu kwa sasa.
Ndio, dunia inaiangalia Tanzania kama kielelezo cha taifa la Kiafrika lililodumu kwa zaidi ya nusu karne bila uwepo wa machafuko na watu kuuana kama ilivyo kwa maeneo mengine ya Afrika.
Tuna kila sababu za kuionyesha dunia, kuwa tunaweza kufanya chaguzi za kidemokrasia bila wenye

Friday, October 23, 2015

ZUMA KUKUTANA NA WANAFUNZI WANAOANDAMANA

 




  Baadhi ya wanafunzi wamepanga kuandamana hadi afisi kuu za serikali Pretoria
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amepangiwa kukutana na viongozi wa wanafunzi wa vyuo leo kujadili maandamano ya wanafunzi yaliyosababishwa na kuongezwa kwa ada ya masomo.
Wanafunzi wamekuwa wakiandamana wiki moja sasa, hasira nyingi zikielekezwa kwa chama tawala African National Congress (ANC).
Mnamo Alhamisi, maelfu ya wanafunzi walikusanyika nje ya makao makuu ya ANC mjini Johannesburg wakitaka elimu itolewe kwa wote bila malipo yoyote.
Vyuo vikuu vimejitetea na kusema vimelazimika kuongeza karo ili kudumisha viwango

Saturday, October 03, 2015

KATIKA KAMPENI MAGUFULI KESHO SINGIDA

 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiombewa Dua na mmoja wa kiongozi wa dini mara baada ya kusimamishwa na Wananchi wa kijiji cha Puma (hawapo pichani),alipokuwa akielekea mkoani Singida mara baada ya kumaliza mkutano wake wa hadhara wa kampeni.
 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akimshukuru kiongozi huyo wa dini kwa kujitolea kumuombea Dua ya heri na afya njema katika nafasi yake ya kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 Mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM Dk. John Pombe Magufuli akiwahutubia wananchi  kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Mnadani Ikungi mkoani Singida jioni ya leo ,wakati akiwaomba  wananchi hao kumpigia kura za ndiyo ifikapo Oktoba 25 mwaka huu katika uchaguzi wa Rais , Wabunge na Madiwani. 



MTOTO MDOGO AWASHANGAZA WANASAYANSI DUNIA NZIMA




Wanasayansi na madaktari nchini Urusi wamestaajabishwa na mtoto mwenye umri wa miezi tisa ambaye mwili wake umekuwa ukitoa maandishi katika lugha ya kiarabu yakinukuu vipande vya maneno katika Quran.

Thursday, October 01, 2015

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI TAREHE 1/10/2015







UNYAMA: WATU WATANO WA FAMILIA MOJA WACHINJWA KAMA KUKU SIMIYU


Watu watano wamefariki dunia papo hapo kwa kukatwa katwa mapanga na kuchinjwa kama wanyama katika kitongoji cha Kisesa kata ya Bugalama wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu.
Watu hao ambao ni wa familia moja walifanyiwa unyama huo kwa kukatwa katwa mapanga sehemu ya shingoni.
Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa polisi Mkoani hapa Gemine Mushy alisema tukio hilo lilitokea juzi majira ya saa 9 ambapo Baba, Mama pamoja na watoto wao 3 waliuawa.
Mushy aliwataja waliofanyiwa unyama huo kuwa George Charles (30) ambaye ni Baba wa familia, Siku John (23) Mama wa Familia na watoto wao ambao ni Mchambi George (7) Tuma George (5) pamoja na Amos George (Miezi 9) wote wasukuma wa kitongoji hicho.


Kamanda Mushy alieleza chanzo kuwa ni mgogoro wa ardhi kati ya marehemu (George) pamoja na Baba yake wa kambo ambaye alinunua kipande cha ardhi alikokuwa akiishi marehemu.
Aliongeza kuwa baada ya tukio hilo jeshi la polisi lilifanya msako na kuwakamata watuhumiwa 3 ambao aliwataja kuwa ni Migata Lusalago (50) Jihelya Migata (30), Solo Kengele (31) wote wasukuma wa kijiji cha Bugalama.
Kamanda mushy alieleza kuwa waliokamatwa ni Baba wa kambo wa Marehemu pamoja na watoto wake wawili ambao ilidaiwa kuwa wameweza kushiriki katika kutenda tukio hilo la kinyama.
Katika hatua nyingine Mushy alisema kuwa uchunguzi wa kina unaendelea kufanyika ili kuwapata wahusika zaidi wa tukio hilo.