
Polisi wa Mali wameingia katika hoteli hiyo
Maafisa
wa serikali ya Mali wamesema sasa hakuna mateka wowote waliosalia katika
hoteli ya Radisson Blu mjini Bamako iliyokuwa imeshambulia asubuhi na
watu wenye silaha huku miili ya watu 18 ikidaiwa kupatikana ndani ya
hoteli hiyo.
Waziri wa
usalama wa Mali Salif Traore ameambia kikao cha wanahabari kwamba watu
wenye silaha walioshambulia hoteli ya Radisson kwa sasa hawazuilii
mateka wowote.

